JUMUIYA
na taasisi za Kiislamu nchini zimemtaka Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera, Uratibu na Bunge), William Lukuvi kujiuzulu haraka iwezekanavyo kutokana
na kauli za uchochezi alizozitoa wakati wa sherehe za kumtawaza Askofu wa
Kanisa la Methodist mjini DodomaHatua hiyo
inatokana na madai ya Lukuvi kwamba endapo muundo wa serikali tatu utapitishwa
nchi itapinduliwa na jeshi na
kwamba Chama cha Wananchi (CUF) Visiwani Zanzibar kinashirikiana na Jumuiya ya Kiislamu ya Uamsho kufanya vurugu za kupinga muungano.
kwamba Chama cha Wananchi (CUF) Visiwani Zanzibar kinashirikiana na Jumuiya ya Kiislamu ya Uamsho kufanya vurugu za kupinga muungano.
Lukuvi pia
katika kauli yake hiyo ambayo imelaaniwa na wananchi wengi huku askofu wa
kanisa hilo akimtaka aombe
radhi na kutubu, alisema kuwa wanaotaka nchi yao
(Wazanzibari) hawawezi kujitegemea, bali wanataka serikali tatu ili wapate
nafasi ya kujitangaza kuwa nchi ya Kiislamu.
Akizungumzia
kauli hizo jijini Dar es Salaam jana mbele ya waandishi wa habari, msemaji wa
jumuiya na taasisi za Kiislamu, Rajabu Katimba, alisema kuwa serikali inatakiwa
ikanushe kwa uwazi na kuwaomba radhi Waislamu na wananchi kwa ujumla juu ya
madai hayo ya Lukuvi.
“Sisi
hatukutarajia waziri mwenye mamlaka makubwa na aliyeaminiwa na rais na
kumwakilisha Waziri Mkuu kutamka kauli chafu na za uchochezi, tena kanisani
dhidi ya Waislamu na Taasisi ya Kiislamu ya Uamsho iliyosajiliwa kihalali.
“Kauli hizi
zina nia ya kuleta chuki, kuwatia woga wananchi na hatimaye kuchafua amani na
kuwanyima haki yao ya kikatiba ya kupendekeza muundo wa katiba wanayoitaka,”
alisema Katimba.
Alisisitiza
kuwa rasimu ya katiba ambayo Lukuvi anasema ikipita italeta matatizo, imetokana
na utafiti wa maoni ya wananchi wa Tanzania Bara na Visiwani ili kuboresha
muungano na kutatua kero mbalimbali zilizodumu kwa miaka 50.
“Kulikuwa na
haja gani serikali kutumia mabilioni ya fedha katika jambo ambalo Lukuvi na chama
chake tayari walishakuwa na mpango wao wa kuendelea na katiba iliyopo hivi
sasa? Kitendo cha kusimama kwa niaba ya serikali katika madhabau ya kanisa na
kueneza propaganda za uchochezi amepata wapi ushahidi juu ya taasisi zetu
kuhusika na hayo?” alihoji.
Kitimba
aliongeza kuwa kitendo cha kuwashambulia wanaoamini katika muundo wa serikali
tatu ni kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete aliyeteua kwa umakini wajumbe wa Tume
ya Mabadiliko ya Katiba iliyokusanya maoni ya wananchi.
“Kumekuwepo
na taarifa za kuzusha kwamba mfumo huo wa serikali tatu ni mpango wa Uamsho ili
Zanzibar iwe nchi ya Kiislamu. Huu ni uongo na upotoshaji,” alisema.
Katimba
alitoa wito kwa viongozi wa dini na serikali kuacha kuwatisha na kuwakashifu
wale wanaotoa maoni yao na kuonyesha kasoro za waliotangulia kwani wao hawakuwa
miungu wasio na upungufu.
“Kwa kufanya
hivyo ni kuzuia uhuru wa watu kutoa maoni yao, pia kuwafanya watu wasitamani
kuishi kwa mawazo yanayoendana na maisha yao ya sasa wayatakayo na badala yake
ni kuwalazimisha kuishi kwa mawazo na mtazamo wa waliopita,” alisisitiza
Katimba.

Chapisha Maoni