Home » » Waziri mkuu wa Mali ajiuzulu

Waziri mkuu wa Mali ajiuzulu

Written By Unknown on Jumapili, 6 Aprili 2014 | 03:06

Waziri mkuu nchini Mali Oumar Tatamy Ly pamoja na baraza lake la mawaziri wamejiuzulu,miezi minane tu baada ya demokrasia kurudi nchini humo kufuatia udhibiti wa eneo la kazkazini uliotekelezwa na wanamgambo wa kiislamu.
Mabadiliko katika serikali yalitarajiwa kufanyika ,lakini taarifa katika mji mkuu wa Mali Bamako,zinasema kuwa
kiwango cha mabadiliko hayo hakikutarajiwa.
Waziri mkuu mpya ,Moussa Mara amekuwa mpinzani mkuu wa rais Boubakr Keita hapo awali.

Bwana Mara aliye na umri wa miaka 39 amekuwa akiitaka serikali kuimarisha usalama katika eneo la kazkazini la nchi hiyo.
Share this article :

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. bentabless.com - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger