Home » » Askofu Mwamalanga awapongeza UKAWA

Askofu Mwamalanga awapongeza UKAWA

Written By Unknown on Alhamisi, 24 Aprili 2014 | 22:31

ASKOFU Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kipentekoste Tanzania, William Mwamalanga, amewapongeza wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) kwa kuondoka bungeni huku akisema wajumbe walibaki wanaendesha ‘bunge la mzaha’.
Akizungumza na Tanzania Daima jana alisema wabunge wa waliobaki wamekuwa wakijadili mambo yasiyo ya maana huku wakiendelea kula kodi za wananchi.

Mwamalanga alisema ni jambo la ajabu na kushangaza kwa mjumbe kutumia Biblia kuwatukana wajumbe waliotoka.
“Bunge linaloendelea sasa ninaliita ni bunge la mzaha na kwamba wananchi wakae chonjo hawatapata chochote kutoka humo, wanachofanya sasa ni kuendelea kula fedha za wananchi kupitia kodi zao,” alisema Mwamalanga.
Alisema CCM imepoteza sifa kutokana na wanachoendelea kufanya bungeni  na kwamba hata baadhi ya viongozi wa dini wamewahama kutokana na kejeli wanazozifanya.

Pia aliwashangaa wajumbe wanaoidharau Tume ya Mabadiliko ya Katiba iliyofanya kazi ya kukusanya mawazo ya wananchi huku akisema dawa iliyopo ni kuwepo kwa serikali ya shirikisho.
Share this article :

Chapisha Maoni

 
Support : Creating Website | Johny Template | Mas Template
Copyright © 2011. bentabless.com - All Rights Reserved
Template Created by Creating Website Published by Mas Template
Proudly powered by Blogger